Maombi ya Kozi ya Mekatroniks

KICTC Diode in the Workshop

MRADI WA KUKUZA AJIRA NA UJUZI-TANZANIA

(EMPLOYMENT AND SKILLS FOR DEVELOPMENT-TANZANIA)

TAARIFA KWA UMMA

FURSA YA MAFUNZO YA UKUZAJI UJUZI KATIKA FANI YA MEKATRONIKI

1. UTANGULIZI

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) inashirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu –

Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kutekeleza

mradi wa Kukuza Ajira na Ujuzi kwa Maendeleo ya Afrika (E4D). Mradi unalenga kuwezesha utoaji

wa mafunzo ya ufundi stadi katika fani ya Mekatroniki (mechatronics), kwa vijana 32 wenye umri

kati ya miaka 15 hadi 35.

Mradi wa E4D unafadhiliwa na Wizara ya Shirikisho la Ujerumani ya Ushirikiano wa Kiuchumi na

Maendeleo (BMZ), Shirika la Ushirikiano wa Maendeleo wa Norway (Norad), Umoja wa Ulaya

(EU) na Shirika la Ushirikiano wa Maendeleo la Korea ya Kusini (KOICA).

Mafunzo yatatolewa katika Chuo cha TEHAMA cha VETA Kipawa kilichopo eneo la Karakata, Dar

es salaam, karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).

2. VIGEZO VYA KUJIUNGA NA FANI

Mwombaji wa mafunzo hayo anatakiwa kukidhi vigezo vifuatavyo:

(i) Uwe raia wa Tanzania.

(ii) Uwe na umri wa kati ya miaka 15 hadi 35 (Idhini ya maandishi ya wazazi/walezi

inahitajika wa watu kati ya umri wa miaka 15 hadi 18 wakati wa mafunzo ya vitendo

viwandani.)

(iii) Awe na ujuzi au uzoefu wa walau mwaka mmoja katika mojawapo ya fani za TEHAMA,

Umeme, Elektroniki au Mekaniko.

(iv) Awe tayari kuhudhuria mafunzo katika Chuo cha TEHAMA cha VETA, KIPAWA katika

muda wote.

Kwa taarifa zaidi, bofya: https://bit.ly/46bfHtX

(1) Comment

  • User Avatar
    vetakipawa 23/12/2023 @ 8:26 pm

    We extend our deepest gratitude to all that applied and wish them the best of luck.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

X